Thursday, 28 September 2017

Uvumilivu wakati wa kusubiri: 2.Tunapaswa kufanya nini wakati tunasubiri majibu ya maombi.  


Karibu kwenye somo la pili la Uvumilivu wakati wa kusubiri majibu
Leo tunaendelea na kuangalia tunachotakiwa kufanya wakati tunasubiri Mungu ajibu tulichomwomba. Kumbuka kuna wakati wa kusubiri, sio mara zote Mungu hujibu muda huohuo ulioomba. 
Wakati huo wa kusubiri, tuangalie tunaweza kuishi vipi ili majibu yakija yatukute tupo tayari kupokea.  


1.    Tuombe Mungu atupe kustahimili.

Yakobo 1:12 “Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa atapokea taji ya uzima, Bwana aliyowaahidia wampendao”

Wakati wa kusubiri majibu ndio wakati kuna majaribu mengi. Adui anakupa mikakati na njia za uongo za kutatua tatizo lako. Kama hujasimama unaweza kuzifuata na utapotea.  Mungu pekee ndiye anaeweza kutupa ustahimili. Roho Mtakatifu ni msaada wetu. Alikuja duniani ili kutusaidia. Tukimtegemea yeye wakati tunasubiri tutaweza kustahimili hadi pale Mungu atakapoleta majibu.


Tuesday, 26 September 2017

Uvumilivu wakati wa kusubiri: Una uvumilivu kiasi gani wakati wa kusubiri majibu kwa Mungu



Ukiomba kwa imani, lazima upate majibu. Yanaweza kuchelewa, yanaweza kuja tofauti na ulivyotegemea, lakini lazima utapata majibu.

Ukipata majibu tofauti, kama hujaomba tafsiri kwa Mungu unaweza kudhani hujajibiwa, na hapo unaweza kukata tamaa, au kumlalamikia Mungu kwanini hajajibu. Unahitaji hekima na utiifu, na uaminifu ili Mungu aukuonyeshe maana ya majibu hayo.

Leo tutazungumzia kile kipindi ambacho unasubiri. Je unavumilia kiasi gani? Uvumilivu wako unakufikisha wapi, unakua unafanya nini wakati wa kusubiri.

Tuangalie aina ya mambo ambayo wengi tunafanya wakati wa kusubiri, baada ya kupata shida au haja fulani, wewe mwanamaombi ukapeleka haja yako kwa Mungu unafanya nini kipindi hicho.

Friday, 15 September 2017

Ushuhuda-Kabla sijamjua Yesu


KABLA SIJAMJUA YESU

Karibuni kwenye ushuhuda wa mpendwa wetu

Mimi ni mwanamke wa miaka 30. Ningependa kushiriki na nyie katika ushuhuda wa maisha yangu. Kabla sijamjua Yesu maisha yangu yalikua yamevurugika. Hakuna kitu nlichokua nafanya kinafanikiwa.  Lakini nikifikiria sasa naona Mungu alikua ananipenda sana. Kuna mambo mengine nilipita kwa uwezo wake bila mimi kujua.

Nilibahatika kusoma na kumaliza chuo. Wakati wenzangu wanahangaika na kazi mimi nilipata tu baada ya kumaliza chuo. Nilibahatika kupata kazi nzuri yenye mshahara mzuri. Lakini kwa sababu nisizozielewa baada ya mwaka mmoja tu nikaacha kazi. Nikakosa hamu ya kuendelea na kazi, nikaondoka huku sijui pa kuanzia.



Pamoja na kwamba nilikua Napata kipato kizuri kwenye kazi lakini niligundua kwenye mwaka mmoja nliofanya kazi, sikufanya kitu chochote cha maendeleo. Nililipa kodi, kuvaa na kula. Nikikaa miezi tisa nyumbani bila kazi, watu wengi walinicheka, nimeacha kazi bila kupata kazi.

Wakati huo nilikua na boyfriend ambaye alikua anakuja kwangu kila weekend. Lakini alikua hanisaidii chochote. Ilikua kama mkosi maana hata yeye alikua anapata kipato kizuri lakini hela yote inaisha bila kujua matumizi yake. Ikifika tarehe za katikati ya mwezi wote hatuna kitu!


Thursday, 14 September 2017

Nguvu ya maombi - Shuhuda



Karibuni kwenye wekeend ya kudeclare nguvu ya maombi. Tunajua kwa namna yoyote kuna hitaji ulilowahi kumwomba Mungu akakujibu. Hata kama ni kitu kidogo kiasi gani, Mungu anapenda shukrani.

Lengo la jambo hili ni kumrudishia Mungu sifa na utukufu kwa baraka anazotupa kila siku.

Pia kuwapa moyo waliokata tamaa. Unaweza kumsaidia mtu yoyote kwa ushuhuda wako. Kama watoto wa Mungu tunapaswa kusaidiana kwa hali yoyote, na moja wapo ya njia ya kusaidiana ni kupeana moyo.



Inawezekana bado una matatizo mengi makubwa ambayo hayajajibiwa, lakini inapaswa kushukuru kwa kila jambo, na hata yale tunayoyaona ni madogo.

Jambo hilo unaloliona ni dogo Mungu anatengeneza njia kupitia jambo hilo na utaona mafanikio ukiwa mwaminifu.



Njia za kututumia ushuhuda wako ni:


Facebook page yetu: Habari Njema Kwetu.

 Tutalinda privacy yako. Hatutaweka jina lako hadharani, au labda upende mwenyewe.

Karibuni sana. Mwisho wa kutoa shuhuda itakua Jumapili Tar 17 September.

Mungu awabariki.


Thursday, 24 August 2017

Unaishi kwa kumtegemea nani


Katika maisha haya unaweza kuishi kwa kutegemea vitu viwili:


1. Kumtegemea Mungu

2. Kutegemea akili zako mwenyewe ( Akili itakutuma kufanya chochote ikiwemo kutegemea nguvu za giza)

 Lakini ukweli ni kwamba kila jambo ulilofanikiwa ni kutokana na neema ya Mungu. Kwa sababu sisi ni watoto wa Mungu. Mungu hana upendeleo katika kutoa baraka. Aliumba watu wote na ana upendo kwa watu wote sawa sawa.

 Kwa hiyo usikate tamaa pale unapoomba, na unaona ambao hawaombi wala hawamjui Yesu wanafanikiwa. Baraka ni zile zile, na mtoaji ni yule yule. Endelea kuamini tu Mungu atamimina baraka zake. Usijaribu kukata tamaa, huwenda siku unayokata tamaa na kuacha kumtegemea Yesu ndio siku aliyopanga Baraka zake zionekane kwako.

 Kuna tofauti kati ya wewe unayemjua Yesu na mwingine, wewe utapata baraka za kudumu, amani na furaha siku zote. Hata katika majaribu utapita kwa ushindi mkubwa na utaona njia ya kutokea haraka, kwa sababu ya nguvu iliyopo ndani yako.

Wednesday, 9 August 2017

Tafuta mafanikio kwa njia sahihi

Habari wapendwa.
Nchi na vyote viijazavyo ni mali ya Bwana. Zaburi 24:11 pamoja na wote wakaao ndani yake. Tukumbuke tunapotafuta mwenye mali ni Mungu, ndiye aliyetuweka hapa na hata akatupa nguvu ya kutafuta.
Ili upate ni lazima umwangalie na umwombe  yeye mtoaji. Usitumie njia nyingine yoyote kama kwenda kwa binadamu mwenzako (mganga) kuomba, kwa namna yoyote hutafanikiwa. Na mafanikio ukiyapata yatakupa stress na si ya kudumu. 

Wazazi ni mfano mzuri wa jinsi Mungu anavyofanya kazi. Mwanao anapohitaji anakuja kwako, anakwambia shida yake. Ndiyo njia rahisi ya yeye kupata hitaji lake.


Ndivyo na sisi inapaswa tumwendee Mungu kumwambia mahitaji yetu. Unataka kupiga hatua kwenye biashara yako, kazi au chochote unachofanya, nenda  kwake mwambie kwa unyenyekevu. Na yeye atakufanyia kama alivyoahidi.


Vitu muhimu vya kukumbuka katika safari yako ya kutafuta 


Monday, 24 July 2017

Jinsi ya kutambua biashara, kazi au huduma Mungu aliyokuwekea

Bwana Yesu asifiwe wapendwa.
Wengi hua tunatamani kuanzisha biashara au kazi ambazo tunataka kuzisimamia wenyewe. Inaweza kuwa vitu kama ufugaji, kilimo, biashara za bidhaa, vyakula, kuandika vitabu, kufundisha, kuhubiri, salons, magari, kuanzisha kampuni mbalimbali nk. Chochote kile unachotamani kufanya mbali na kazi yako ya kuajiriwa. Naamini ni watu wachache wasio na ndoto za kufanya mambo yao binafsi ya kuingiza vipato.

Faida za kazi/biashara binafsi.

  1. Kujiridhisha kuwa unaweza kufanya jambo mwenyewe, (personal satisfaction). Inakupa kujiamini unaweza kufanya jambo lako peke yako kwa mafanikio na likakuingizia faida ya kiuchumi na kwa jamii.

  1. Unajisikia kutimiza karama au kipaji unachoamini umepewa na Mungu. Kama una karama ya kuandika siku ukifanikiwa kutoa kitabu chenye kuleta faida kwa jamii utajisikia furaha kua umetimiza karama uliyopewa.

  1. Kuleta faida kiuchumi, kipato kuongezeka. Ukifanikiwa kufanya jambo peke yako na ukafanikiwa kupata faida ni furaha sana.

  1. Kupata mwelekeo mzuri wa maisha. Haimaanishi anayetegemea mshahara peke yake hana mwelekeo, lakini ni jambo kubwa zaidi ukiweza kutumia akili yako kuanzisha kitu na kukisimamia, na kuleta faida na matokeo chanya kwa jamii. Hata waliokuajiri walianza na wazo kama hilo, wakaweza kuendelea hadi kufanikiwa kuajiri.

  1. Kujiamini. Unajisikiaje kuwa bosi wako mwenyewe? Lazima kuna furaha na kujiamini kuwa umeweza.

Sasa  mara nyingine tunapata shida kuanzisha biashara au kazi za kujitegemea. Kwa sababu ya mambo mbali mbali ikiwemo  kutokujiamini, adui kufunga milango, aibu, uoga, malezi nk. Hapa chini kuna mwongozo wa mambo ya kufanya kabla ya kuanzisha biashara au kazi ya kujitegemea (self employment).

Tuesday, 18 July 2017

Jinsi ya kupanga ratiba yako ya kila siku ili ufanye yote kwa msaada wa Mungu

Bwana Yesu asifiwe wapendwa.
Katika safari ya mafanikio tunakumbana na mambo mengi. Wakati mwingine kazi zinakua nyingi au masomo yanakua magumu muda wote tunakimbizana. Yote hii ni kufanikisha maendeleo binafsi (personal development).

Katika hali ya kawaida tukifikiria kufanikiwa tunafikiria maisha mazuri, nyumba,  familia nzuri unayoweza kuitimizia kila kitu,, magari, kua na uchumi imara, yaani kutopungukiwa na kitu. Tuna maono mengi na tunajaribu kwa nguvu zetu zote kufanya kazi kwa bidii ili tuyafikie.

Lakini katika yote hayo, nafasi ya Bwana wetu Yesu ipo? Inawezekana ipo, jumapili unahudhuria ibada na bible study. Lakini je inatosha.

Katika shughuli zetu inapaswa kumuangalia Mungu kwanza, halafu uone kupitia yeye (see through Him). Asubuhi hii unapoanza kazi/biashara/masomo yako, muangalie kwanza Mungu, tambua ukuu wake, tafakari jinsi alivyokufanyia mambo mengi, na alivyo msaada kwa kila unachofanya.

Kisha anza kazi yako. Kwenye kila changamoto unayokutana nayo leo, mkumbushe ahadi zake, amesema ukimwomba kitu kwa imani atakupa, amesema hatakuacha.. endelea na kazi yako huku nafsi yako ikiwa imejazwa uwepo wa Mungu.

Unawezaje kufanya hivyo?

Sunday, 16 July 2017

Usitumie muda wako wote kuwaza, mwambie Mungu


Mara nyingi hua tunapoteza muda mwingi sana kuwaza matatizo.  Mtu mmoja unaweza ukashambuliwa na mambo mengi hadi ukakata tamaa ya maisha. Matatizo yapo mengi, na ni jukumu letu kutafuta njia ya kuyatatua.

Tunachokosea ni pale tunapojaribu kusolve kitu kimoja kimoja kwa kutumia akili zetu wenyewe.  Sina maana usijaribu kutafuta suluhisho la matatizo yako, lakini je unaweza? Baadhi ya watu wanapata mawazo kwa sababu ya vitu vidogo sana na anajikuta anaharibu mambo mengine kwa sababu hiyo.

Tuangalie mstari huu, Waefeso 4:6 “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.”

Unadhani Mungu hatambui mambo unayopitia? Anajua kabisa, na pengine anasikitika unavyotumia njia tofauti kusolve tatizo lako. Ndio maana tunakumbushwa kuwa tusijisumbue kwa jambo lolote. Hapa hamaanishi utulie bila kujua suluhisho la shida yako. Ametoa njia mbadala ya kujisumbua, ni kusali, kuomba na kushukuru, haja zetu zijulikane na Mungu.

Mungu akishaona umempelekea haja yako  atakupa mwongozo wa kutatua. Mstari wa 7 “Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu”

Mungu akishajua haja yako atakupa amani yake ipitayo akili zote ikuhifadhi moyo wako na nia yako. Hutakosa amani tena na kuwaza kupitiliza kwa sababu tayari una amani ya Mungu na  atakuonyesha njia ya kumaliza shida yako.

Kuna msemo unaosema 'pray until something changes’ yaani omba hadi uone madadiliko. Usikubali adui akujazie matatizo kichwani uone umebeba mzigo ambao hakuna anaeweza kubeba. Hiyo ni trick ya kukufanya uone Mungu hakusaidii. Mungu anataka useme nae tu na uamini kua atafanya, nae atafanya.

Wednesday, 12 July 2017

Jinsi ya kuulinda moyo wako usiumizwe

Wote tunajua kuumizwa moyo katika mahusiano. Kwa namna moja au nyingine kila mtu ameumizwa na na mtu mwengine,  kwenye mahusiano mbalimbali, kama urafiki, ndoa, kazi, biashara nk.  Unapofanyiwa jambo baya kwenye uhusiano moyo unaumia. Kuna hisia unapata ya moyo kukosa amani, kuuma, kuwa na wasiwasi na kukosa kujiamini.  Unaweza ukaumia kwa muda na baadae unapoa.
Kwa nini tunaumia?
Ni pale unapotegemea kupata vitu fulani kwa mwenzako (mume, mke, mchumba,rafiki, mzazi nk), halafu unapata kinyume na ulivyotegemea. Au anakufanyia jambo baya ambalo hukutegemea. Mfano, mke au mume anakua na uhusiano nje ya ndoa. Ukijua lazima itauma sana. Au rafiki anakusaliti, au kukudhulumu, lazima moyo unakuuma kwa sababu ni kinyume na ulivyotegemea.

Kwa nini tunategemea mambo mazuri kutoka kwa wenzetu?
Ni kwa sababu tumejenga uaminifu kwao. Unamwamini mume au mke wako sana kwa hiyo unaamini hataweza kukufanyia jambo baya. Pia ni kwa sababu ya ukaribu tulio nao kwao. Una rafiki wa karibu sana mnajuana na kutunziana siri, unajua kwa ukaribu mlio nao hawezi kukuumiza.

Ni nini hua kinabadilika?

Tuesday, 11 July 2017

Jinsi ya kumiliki ukuu wa Mungu

Karibu tujifunze pamoja
Mara nyingi tunapopata shida tunasahau mema yote Mungu aliyotufanyia.  Na baada ya kupita shida hua tunasahau jinsi Mungu alivyotupitisha. Ni udhaifu tulio nao.
Tuangalie mfalme Daudi alivyofanya katika 2 Samweli 22. Daudi baada ya kushinda vita ya wafilisti, alimsifu Mungu na kuelezea jinsi alivyomwokoa. Huu ni mfano mmoja tu kati ya mingi ya mfalme Daudi akiabudu na kusifu baada ya kushinda.

Katika neno hili Daudi amemwelezea Mungu kwa kutumia vitu vyenye nguvu. Mfano, Bwana ni jabali langu, ngome yangu,mwokozi wangu,mwamba wangu, ngao yangu nk. Angalia alivyojimilikisha ukuu wa Mungu. Kila wasifu aliompa Mungu aliufanya wake kwa kusema “yangu”, “wangu”. (Ngome yangu, mwokozi wangu..)
Mfalme Daudi hakujali  alipitia mangapi, alichojali wakati huo ni jinsi Mungu alivyomwokoa. Ni dhahiri alikua akiongea maneno hayo akiwa mwenye furaha. Na alikua ameamini kabisa kuwa Mungu ndiye aliyefanya, akaona anastahili sifa zote alizompa.
Katika maisha yetu ni muhimu tujue jinsi ya kumiliki ukuu wa Mungu. Ukijua Mungu ndiye anaekuongoza na kukupa vyote ulivyo navyo, imani yako haitapungua hata wakati wa majaribu.

Ni kawaida kwetu kujiuliza maswali na kumlalamikia Mungu tukihisi amenyamaza. Lakini ukishajihakikishia na kuamini Mungu ndie amekufikisha ulipo, hutaona amekuacha unapopitia shida. Hii ndio maana ya kuufanya ukuu wa Mungu ngao yako.

Tunawezaje kuumiliki ukuu wa Mungu?

Friday, 7 July 2017

Weekend ya kushukuru: Jinsi ya kumshukuru Mungu wakati wa shida

Karibu kwenye weekend ya kushukuru.

Ni ngumu binadamu kumshukuru Mungu wakati wa matatizo na changamoto. Mara nyingi tunaishia kumlalamikia Mungu na kumuuliza maswali mengi, kwanini tuyapitie tunayopitia.
Ni ngumu sana mfano ukiwa na mgonjwa au ukiondokewa na mpendwa ukamshukuru Mungu. Hua tunajiuliza maswali mengi pasipo na majibu.

Ayubu alipitia wakati mgumu sana wa kuondokewa na watoto, mali zake zote mke, na kila alichokua nacho. Alifika wakati akasema, “Na ipotelee mbali ile siku niliyozaliwa mimi, Na ule usiku uliosema, Mtoto mume ametungishwa mimba.  Siku hiyo na iwe giza; Mungu asiiangalie toka juu, Wala mwanga usiiangazie”
Ayubu 3:3‭-‬4

Alilalamika kwa muda mrefu akilaumu kila kitu na kujibishana na marafiki zake. Akizungumzia jinsi alivyo mwenye haki mbele za Mungu.  Na Mungu alimsikiliza wakati wote huo. Akaamua kumjibu;  

Wednesday, 5 July 2017

Jinsi ya kuepuka wivu ili ufanikiwe


Bwana Yesu asifiwe!

Wivu ni jambo linalosumbua watu wengi. Watu wanasema kuna wivu wa aina mbili. Wivu wa maendeleo (kutaka kujifunza) na wivu mbaya wa kuchukia pale mtu mwingine  anapoendelea.
Habari ya wivu imeongelewa kwenye  Zaburi 73.

Katika jamii kuna mtu anaeweza jambo fulani kuliko mwingine, kimwili au kiroho, kwa sababu Mungu ametugawia karama mbali mbali tofauti. Kila mtu amepewa karama yake.

Yakobo na Esau, (Mwanzo 25: 21-34) Walianza kushindana toka tumboni mwa mama yao Rebeka (mst 22). Wote walikua wameandikiwa baraka,ya kua mataifa makubwa, lakini Mungu alisema watafarakana toka tumboni. 

Ndivyo ilivyo hata maisha ya sasa, kuna mashindano, kuna ambae ataonekana bora kwa jambo fulani kuliko mwingine. Lakini kila mtu ana kitu anachoweza kufanya.
 Tufanyaje ili tuweze kufanyia kazi uwezo wetu badala ya kuonea wivu wengine?