Karibu kwenye somo la pili la Uvumilivu wakati wa kusubiri majibu
Leo tunaendelea na kuangalia tunachotakiwa kufanya wakati tunasubiri Mungu ajibu tulichomwomba. Kumbuka kuna wakati wa kusubiri, sio mara zote Mungu hujibu muda huohuo ulioomba.
Wakati huo wa kusubiri, tuangalie tunaweza kuishi vipi ili majibu yakija yatukute tupo tayari kupokea.
1.
Tuombe
Mungu atupe kustahimili.
Yakobo 1:12 “Heri mtu astahimiliye
majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa atapokea taji ya uzima, Bwana
aliyowaahidia wampendao”
Wakati wa kusubiri majibu ndio wakati kuna majaribu
mengi. Adui anakupa mikakati na njia za uongo za kutatua tatizo lako. Kama
hujasimama unaweza kuzifuata na utapotea.
Mungu pekee ndiye anaeweza kutupa ustahimili. Roho Mtakatifu ni msaada
wetu. Alikuja duniani ili kutusaidia. Tukimtegemea yeye wakati tunasubiri
tutaweza kustahimili hadi pale Mungu atakapoleta majibu.

