Tuesday, 26 September 2017

Uvumilivu wakati wa kusubiri: Una uvumilivu kiasi gani wakati wa kusubiri majibu kwa Mungu



Ukiomba kwa imani, lazima upate majibu. Yanaweza kuchelewa, yanaweza kuja tofauti na ulivyotegemea, lakini lazima utapata majibu.

Ukipata majibu tofauti, kama hujaomba tafsiri kwa Mungu unaweza kudhani hujajibiwa, na hapo unaweza kukata tamaa, au kumlalamikia Mungu kwanini hajajibu. Unahitaji hekima na utiifu, na uaminifu ili Mungu aukuonyeshe maana ya majibu hayo.

Leo tutazungumzia kile kipindi ambacho unasubiri. Je unavumilia kiasi gani? Uvumilivu wako unakufikisha wapi, unakua unafanya nini wakati wa kusubiri.

Tuangalie aina ya mambo ambayo wengi tunafanya wakati wa kusubiri, baada ya kupata shida au haja fulani, wewe mwanamaombi ukapeleka haja yako kwa Mungu unafanya nini kipindi hicho.



Mambo ambayo wengi tunafanya wakati wa kusubiri majibu.

1.    Wengi sana hukata tamaa. Tunaacha kuomba, tunaendelea na maisha yetu, tunasema tunamwachia Mungu. Hapo ni kama kumsusia Mungu, huombi lakini unasema unamwachia. Mara nyingine unaweza ukaona majibu, lakini elewa kabisa sio kwa sababu ulimwachia Mungu, ni kwa sababu Mungu wetu ni wa neema sana, akaona mtoto wake asipate shida, akaamua kukupa haja yako.

2.    Kulalamika. Hapa unaweza ukawa unaomba lakini kwa kulalamika. Wakati mwingine kwa kulia sana na kupiga kelele. Inawezekana Mungu akasikia na akajibu, lakini elewa kabisa hajajibu kwa sababu umelalamika au kulia sana. Ni kwa sababu ya Neema yake kwetu.

3.    Matendo ya mwili. Ukiwa unasubiri majibu, unakua mtoaji sana huku ukiamini kwa kufanya hivyo ni kumfanya Mungu akupe majibu yako. Mara nyingine hata watumishi wanasisitiza hilo, kwamba toa sadaka kiasi fulani, na utaona majibu yako. Naomba uelewe kutoa ni jambo zuri sana na linalompendeza Mungu sana. Lakini unatoa kwa malengo gani. Angalia usitoe kwa kumhonga Mungu, kumbuka yeye ndie alitoa vyote tulivyo navyo. Ni mmilikia wa kila kitu, hakuna unachoweza kumpa ili umfanye akusaidie.

Kwa hiyo, tunatoa ili kumwonyesha Mungu kuwa tunamwamini kwa vyote tulivyo navyo, tunaamini yeye ndiye Mungu, ndiye mfalme wamaisha yetu. Hatutoi ili afanye jambo fulani, hiyo ni wrong motive. Usiende mbele zake huku ukimkumbusha  ulitoa sadaka kwa ajili ya majibu ya maombi yako.





Ni vyema tujue namna ya kukaa uweponi kwa Mungu wakati wa kusubiri majibu ya maombi yetu. Tunaweza kuwa tunapitia mateso wakati wa kusubiri, hayo yanakujenga ili uweze kuvumilia zaidi, usitetereke uwe na uwezo wa kukabiliana na jambo lolote.



Somo la pili la uvumilivu litaendelea. Tujue jinsi ya kuweza kuvumilia, tunatakiwa kufanya nin wakati wa kusubiri, na mengine mengi.



Ubarikiwe sana.




No comments:

Post a Comment